Thursday, March 22, 2012

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU UCHAGUZI
WA VIONGOZI WA CHAMA CHA MPIRA WA MIGUU MKOA WA KAGERA (KRFA).
 TAREHE 21/03/2012
 
1.                   Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linawajulisha wadau wa soka kwamba uchaguzi wa viongozi wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa Kagera ulifanyika tarehe 17 Machi 2012, Bukoba mjini kama ulivyokuwa umepangwa. Uchaguzi huo ulifanyika kwa mujibu wa Katiba ya KRFA na Kanuni za Uchaguzi za wanachama wa TFF.
 
2.                   Viongozi waliochaguliwa kwenye Kamati ya Utendaji ya KRFA ni hawa wafuatao:
 
(i)                   Mwenyekiti:                                                 Ndg. Jamal E. Malinzi
(ii)                 Makamu Mwenyekiti:                                   Ndg. Alex Raphael Gashaza
(iii)                Katibu Mkuu:                                               Ndg. Salum H. Umande
(iv)               Mweka Hazina:                                           Ndg. Adolf Martin Mahuguli
(v)                 Mjumbe wa Mkutano Mkuu TFF:                   Ndg. Peregrinius A. Rutayuga
(vi)               Mjumbe- Mwakilishi wa Vilabu:                     Ndg. Didas David Zimbihile
(vii)              Wajumbe- Kamati ya Utendaji:          -           Ndg. Abubakari Kazinja
-           Ndg. Dionise Magezi
-           Ndg. Ezekiel Geofrey Samson
 
3.                   TFF inawashukuru wadau wa soka Mkoani Kagera, hususan, wajumbe wa Mkutano Mkuu wa KRFA na Kamati ya Uchaguzi ya KRFA kwa kuheshimu na kuzingatia Katiba ya KRFA,  Kanuni za Uchaguzi za wanachama wa TFF na kwa ushirikiano mkubwa walioutoa kwa Kamati ya Uchaguzi ya TFF, hivyo kufanikisha kufanyika kwa uchaguzi wa KRFA kama ulivyopangwa. Ni matumaini ya TFF kuwa wadau wa soka Mkoani Kagera wataendelea kushirikiana na TFF kuendeleza soka katika Mkoa wa Kagera.
 
Sunday Kayuni
KAIMU KATIBU MKUU

No comments:

Post a Comment