Thursday, March 22, 2012

bomoa bomoa kupisha kituo kikuu cha mabasi yaendayo kasi kuzikumba nyumba za shirika la reli na bandari gerezani jijini dar alfajiri ya leo

 Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mhe.Meck Sadick akiongea na waandishi wa habari jioni ya leo juu ya bomoa bomoa ya nyumba za mtaa wa Gerezani zilizokuwa zinamilikiwa na shirika la Reli pamoja na mamlaka ya bandari. Zoezi hilo litafanyika kuanzia kesho saa kumi na moja alfajiri, pia amewataka wakazi wanaoishi maeneo hayo wawe wameishahama katika maeneo hayo kabla zoezi hilo kufanyika. Amesema zoezi hilo litafanywa na kampuni ya Yono action mart ili kupisha ujenzi wa kituo kikuu cha mabasi yaendayo kasi.

Wawakilishi kutoka wakala wa serikali (DART)pamoja na (YONO ACTION MART)wa kwanza kushoto ni mkurugenzi mtendaji wa (DART) Bw.Cosmas Takule. Katikati  ni Mkurugenzi mtendaji wa Yono Bi Scholastica Kevela na kulia Afisa masoko Yono action mart Bw. Joseph Assey. 
(PICHA NA PHILEMON SOLOMON)

No comments:

Post a Comment