Thursday, March 22, 2012

KUFUNGWA KWA MASHINDANO YA UCHORAJI NA KUTOA ZAWADI

Siku ya Jumamosi tarehe 24/03/2012 kutakuwa na kufungwa na kugawa zawadi kwa washindi wa Mashindano ya Uchoraji yaliyobeba kichwa cha Habari cha Miaka 50 ya Taifa yakishindanisha Tasisii za Elimu kuanzia shule za awali ,Msingi,Sekondari na Vyuo ,mashindano yaliyoandaliwa na Image Profession.

Hafla ambayo itatanguliwa na maonyesho ya picha za washiriki wa shindano pamoja na kuonyesha picha za wachoraji wazoefu kuanzia saa 11 :00 (Saa Tano)asubuhimpaka saa 14 :00(Saa Nane)Mchana kwenye Ukumbi wa Jumba la Makumbusho ya Taifa makabala na Chuo cha Fedha(I.F.M.)

Njoo ushuhudie Vipaji katika Sanaa za Uchoraji ,njoo uwape moyo Washiriki na pia uweze kujifunza mambo mengi yahusuyo sanaa hii ya uchoraji.
Pia Njoo ujuwe kichwa cha habari cha Mashindano ya Mwaka huu 2012.

WENU KATIKA UJENZI WA SANAA NA MICHEZO
Image Profession & iP Sports Club

kitabu kipya cha simulizi kiko mitaani


JINA LA KITABU: MALIPO NI HAPAHAPA
      MTUNZI:  ADELA DALLY KAVISHE 
Adela Daly Kavishe (pichani)   ni mtangazaji wa radio passion FM ambayo inarusha matangazo yake jijini Dar es salaam Ninayofuraha kukamilisha kitabu cha simulizi cha MALIPO NI HAPAHAPA ambacho kimebeba simulizi tatu za kusisimua ikiwemo simulizi inayoitwa DADA YANGU,MAMA MDOGO pamoja na simulizi iliyobeba jina la kitabu MALIPO NI HAPAHAPA 
 Kitabu cha Malipo ni Hapahapa na simulizi nyingine za maisha kinaonyesha hali halisi ya maisha tunayoishi, matatizo tunayokutana nayo na namna ya kutatua matatizo tunayoyapata kwa wakati huo. Pia kwa kusoma kitabu hiki utajifunza mengi kwani kinatoa  picha halisi ya maisha yetu ya kila siku.
Ndani ya kitabu hiki nimezungumzia maisha na mapenzi katika mtazamo halisi na pia kinaonyesha namna mapenzi yanavyoweza kuyageuza maisha kuwa machungu na mafupi. 
Ukianza kusoma kitabu hiki hutakiacha hadi ukimalize kwani hadithi zilizomo zimesheheni matukio ya kusisimua ambayo moja kwa moja yanalenga maisha yetu ya kila siku.
Kupitia vitabu vya simulizi za maisha kama vile kitabu hiki, tunajifunza mambo mengi ambayo yanatusaidia kuishi katika mazingira tofauti ikiwa ni katika shida au raha na hata kujua namna ya kuishi na watu wanaotuzunguka.
Utapata kitabu hiki kwa  bei ya sh 5000 tu.
 Kwa mawasiliano kuhusu upatikanaji wa kitabu hiki.
Tafadhali tumia no zifuatazo +255652343430 au +255752817444
Au kavisheadela@yahoo.com  Unaweza pia kuingia humu http://www.adeladallykavishe.blogspot.com 

bomoa bomoa kupisha kituo kikuu cha mabasi yaendayo kasi kuzikumba nyumba za shirika la reli na bandari gerezani jijini dar alfajiri ya leo

 Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mhe.Meck Sadick akiongea na waandishi wa habari jioni ya leo juu ya bomoa bomoa ya nyumba za mtaa wa Gerezani zilizokuwa zinamilikiwa na shirika la Reli pamoja na mamlaka ya bandari. Zoezi hilo litafanyika kuanzia kesho saa kumi na moja alfajiri, pia amewataka wakazi wanaoishi maeneo hayo wawe wameishahama katika maeneo hayo kabla zoezi hilo kufanyika. Amesema zoezi hilo litafanywa na kampuni ya Yono action mart ili kupisha ujenzi wa kituo kikuu cha mabasi yaendayo kasi.

Wawakilishi kutoka wakala wa serikali (DART)pamoja na (YONO ACTION MART)wa kwanza kushoto ni mkurugenzi mtendaji wa (DART) Bw.Cosmas Takule. Katikati  ni Mkurugenzi mtendaji wa Yono Bi Scholastica Kevela na kulia Afisa masoko Yono action mart Bw. Joseph Assey. 
(PICHA NA PHILEMON SOLOMON)

rais kikwete afunga maonesho ya maadhimisho ya wiki ya maji kitaifa mkoani iringa leo

 Mto Ruaha ukionekana kutoka juu ukitiririsha maji ambao Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ameahidi kuchukua hatua madhubuti za kuunusuru mto huo dhidi ya uharibifu ili kuleta tija zaidi katika kilimo cha umwagiliaji na uzalishaji umeme.Rais Kikwete ametoa ahadi hiyo wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya maji iliyofanyika kitaifa Mkoani Iringa .
Rais Kikwete akisalimiana na baadhi ya wananchi waliohudhuria kilele cha maadhimisho ya wiki ya maji kilichofanyika kitaifa katika uwanja wa Michezo wa Samora mkoani Iringa
 
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiangalia bustani ya mfano inayotumia utaalamu wa kumwagilia kwa matone(drip Iririgation) wakati wa maonyesho yaliyofanyika katika Uwanja wa michezoi wa Samora mkoani Iringa
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo ya jinsi ya kutibu maji kutoka kwa mtaalamu wakati alipotembelea mabanda ya maonyesho katika uwanja wa michezo wa Samora mjini Iringa. Picha na Freddy Maro 
Rais Jakaya Kikwete akimsikiliza Mkurugenzi Msaidizi wa Maji Vijijini Wizara ya Maji na Umwagiliaji Bw. Amani Mafuru wakati akitoa taarifa ya wiki ya maji mkoani Irinaga leo, Kushoto ni Naibu Waziri wa maji Mh. Grayson Rwenge.
 Rais Jakaya Kikwete akisikiliza maelezo ya Mkurugenzi wa maji Mijini Wizara ya Maji na Umwagiliani Bw.Yohana Monjesa katika kilele cha wiki ya maji mkoani Iringa.
Mtaalam wa Maendeleo ya Jamii katika mradi wa wa Mazingira katika Ziwa Victoria BwRaymond Mariki akitoa maelezo ya utekelezaji wa majukumu ya mradi huo mbele ya Rais Jakaya Kikwete katika maonyesho ya wiki ya maji Mkoani Iringa yaliyomalizika leo.

Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wakuu na na wafadhili (mstari wa mbele) sambamba na kamati ya maandalizi ya maadhimisho ya wiki ya maji Kitaifa yalifikia tamati leo na kufungwa rasmi na Rais Kikwete mapema leo jioni kwenye Uwanja wa Samora mkoani Iringa.

Rais Jakaya Kikwete akikabidhi cheti cha shukrani kwa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) na Kupokelewa na Mkurugenzi wake wa Mahusiano na Mawasiliano Teddy Mapunda. Pia SBL walipokea Cheti cha ushiriki wa maonesho hayo. 
 Baadhi ya viongozi  wa Serikali na wageni waalikwa wakiwa ameketi jukwaa kuu
Rais Kikwete akielekea kukagua Mabanda ya maonesho ndani ya Uwanja wa Samora mapema jioni hii,ambapo Rais Jakaya Kikwete leo amefunga Maadhimisho ya Wiki ya Maji Kitaifa Mkoani Iringa. Pamoja na kuhutubia katika kilele hicho pia Rais alipata fursa ya kutembelea mabanda mbalimbali ya maonesho ya watoa huduma za maji na wadau mbalimbali wa maji nchini.
Pichani ni Rais Kikwete akisalimiana na Mkurugenzi wa Mahusiano na Mawasiliano wa kampuni ya bia ya Serengeti Bi Teddy Mapunda mara baada ya kulitembelea banda hilo,ambao ndio wadhamini wakuu wa maadhimisho hayo ya mwaka huu yaliyofanyika uwanja wa Samora Mjini Iringa. na pichani kati ni Meneja Miradi Endelevu na Uwajibikaji wa SBL, Nandi Mwiyombela.
Mkurugenzi wa Mahusiano na Mawasiliano wa kampuni ya bia ya Serengeti Bi Teddy Mapunda akitoa maelezo mafupi kwa Mgeni rasmi,Mh Rais Kikwete  mara baada ya kulitembelea banda hilo.

Mh. Lowassa akuatana na Walimu wa Shule ya Sekondari ya Engutoto,Monduli leo kujadili hali ya elimu ya shule hiyo

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akizungumza kwa kusisitiza wakati wa mkutano wake na Walimu wa Shule ya Sekondari ya Engutoto,Wilayani Monduli kuhusiana na hali ya elimu katika shule hiyo kutoridhisha na kupelekea wanafunzi wengi wa shule hiyo kufeli kwenye mtihani wa taifa wa kidato cha nne.Mkutano huo umefanyika leo shuleni hapo,ambapo walimu wa shule hiyo walitoa changamoto mbali mbali wanazokabiliana nazo.Mh. Lowassa amewaasa walimu wa Shule hiyo kuwa wafanye kazi kwa juhudi ili kuwaandaa vijana wa taifa la baadae.Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shule hiyo,Bw. Joseph Lukumay.
Afisa Elimu Wilaya ya Monduli,Bw. Shaaban Mngunye (kushoto) akifafanua jambo kwa Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa (wa pili kulia) wakati wa mkutano na Walimu wa Shule ya Sekondari ya Engutoto,Wilayani Monduli.Kulia ni Mkuu wa Shule hiyo,Mwl. Ally Muyago na wa pili kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shule hiyo,Bw. Joseph Lukumay.
Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Shule ya Sekondari ya Engutoto,Bw. Joseph Lukumay akitoa maelezo mafupi na kuwataka walimu wa shule hiyo kuanza kuzungumzia ni kwanini shule yao imefanya vibaya kwenye mtihani wa taifa wa kidato cha nne.
Mwalimu wa Shule ya Shule ya Sekondari ya Engutoto iliyopo Wilayani Monduli Mkoani Arusha akitoa taarifa fupi ya shule kwa Mh. Edward Lowassa ambaye ni Mbunge wa Jimbo hilo la Monduli,wakati wa mkutano wake na Walimu wa Shule hiyo kuhusiana na hali ya elimu katika shule hiyo kutoridhisha na kupelekea wanafunzi wengi wa shule hiyo kufeli kwenye mtihani wa taifa wa kidato cha nne.
Walimu wa Shule ya Engutoto iliyopo Wilayani Monduli Mkoani Arusha,wakizungumzia changamoto mbali mbali wanazokabiliana nazo katika kazi yao ambapo wengi wamedai kuwa inachangia kwa kiasi fulani kudhorota kwa elimu katika shule hiyo.

NIHILENT announces strategic partnership designed to mutually benefit local companies scale up and grow their business.

Mr Minoo Dastur, Chief operating officer and Director of  Nihilent (centre) speaks to reporters today at the Holiday Inn in Dar es salaam today. Right is Mr   Ravi Teja, Vice President of Global Consulting  and right is Mr  Davie Kahwa the  Chief Executive O fficer of Equip. 

NIHILENT, aleading global consulting and solutions intergration Company and EQUIP GRC, an advisory firm that provides governance, risk management and internal audit transformation solution, today announced a strategic partnership designed to mutually benefit both companies to scale up and grow their business.

This strategic partnership will address the requirement for local capability builiding around sound business management practices, especially in the area of Business and information Technology consulting. This partnership is a direct response to the pro- investment and pro-growth policies and " New Vigor, New Zeal, and New speed" theme pursued diligently by the progressive government which seeks to unleash Tanzania's talent growth potential. 



While Equip brigs with it leading practices in corporate governance, risk management, regulatory compliance and internal audit transformation , Nihilent brigs hard rigor and  plentiful experience into effective deployment through its competence around corporate strategy execution capability. 


Equip and  Nihilent will combine their expertise to address the business challenges facing organizations in the Financial Services, Government and state-run enterprises and Supply chain and Logistics. 

BODI YA TASAF WAMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA PEMBA

 Mkuu wa mkoa wa pemba Mh Juma kassim Tindwa ( katikati mwenye suti nyeupe) akiwa katika picha ya pamoja  na  ujumbe wa bodi ya Mfuko wa maendeleo ya jamii ulio chini ya ofisi ya Rais (TASAF) ulipomtembelea ofisini kwake nakumfahamisha kazi wanayo ifanya kisiwani hapo
Bi Hadiya Mwinyi Suedi akipiga ngoma huku akiongoza kikundi cha Msondo  kuburudisha  ujumbe wa bodi ya TASAF  pamoja na wafanyakazi wa taasisi hiyo walipofika katika kisiwa cha Pemba kwa ajili ya kukagua miradi inayo dhaminiwa na TASAF