Wednesday, March 21, 2012

JENGO LA CM PLAZA LAZINDUA TEKNOLOJIA MPYA YA KUFANYA USAFI MAJENGO MAREFU

 Mkurugenzi wa kampuni ya Equilibrium Rope Access Bw. Abdulkarim Tumba akipanda juu kwa ajili ya kusafisha vioo kwa kutumia teknolojia ya Rope Access ambayo ni mpya kwa hapa nchini. Aliongeza kuwa ni vyema Watanzania wenye majengo wakajitokeza kuitumia teknolojia hii ambayo ni salama. Na leo kwa mara ya kwanza tokea teknolojia hiyo imeingia nchini Tanzania wameifanya katika Jengo la CM Plaza lililopo  Mikocheni jijini Dar es Salaam.
 ...Akielekea juu kwa ajili ya kuanza kusafisha jengo hilo; ambapo usafi unafanyika kwa ustadi kabisa.
 Muonekano wa jengo huku akionekana Bw. Abdulkarim Tumba akiendelea na usafi.
 Akiendelea na usafi ambapo haitaji vifaa vingi wala umeme na ni haraka na salama.
Jengo la CM Plaza kama linavyoonekana wakati likifanyiwa usafi.

No comments:

Post a Comment