Wednesday, March 21, 2012

balozi wetu mpya nchini kenya awasili nairobi tayari kuanza kazi

 Mh. Balozi Batilda S. Burian aliwasili kwenye kituo chake kipya cha kazi Jumatatu  na kupata mapokezi makubwa kutoka kwa Maafisa wa Ubalozi na Watumishi wengine na pia kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kenya.

Mh. Balozi akipokea Ua kutoka kwa Bibi Anne Waweru, mmoja wa Watumish kutoka Ubalozi wa Tanzania, Nairobi.

 Mh. Balozi akisalimiana na baadhi ya Watumishi wa Ubalozi.  Hapa anasalimiana na Bibi Namweta Nguve, Receptionist.  Wengine wanaonekana ni Bibi Beatrice Mwambene, Mwambata Utawala( aliyebeba ua) na Major Mapunda.
 Mh. Balozi akisalimiana na Madereva wa Ubalozi kutoka kushoto ni Bw. Oppo, Bw. Amos na Bw. Moses ambaye ni dereva wa Mh. Balozi.

 Mh. Balozi Batilda S. Burian akisalimiana na Balozi Mdogo Bw. Yahaya Haji Jecha.
 Maafisa na Watumishi wengine wa Ubalozi wakisubiri kumpokea Mh. Balozi Nairobi Safari Club ambako alifikia  kwa muda.  

Mh. Balozi akitoa salaam rasmi kwa Watumishi wote wa Ubalozi mara baada ya kuwasili hotelini.

No comments:

Post a Comment