Monday, March 19, 2012

hoja ya haja: Wazazi twende na wakati

Ndugu Michuzi na wasomaji, hamjambo!
Kuna jambo katika jamii zetu za kiafrika, lahitaji kuongelewa na kubadilishwa kwani haliendani na wakati. Jambo hili ni lile la kumtoza mahari kijana anayeoa. Wengi mtakubaliana nami kuwa watu huoana kwa kupendana na kwa hiari yao (asilimia kubwa na siyo ile ya kulazimishwa, 'arranged marriage'), kufuatia  makubaliano yao wenyewe hatimaye kuwajulisha wazazi/walezi. Uamuzi huu huleta furaha kubwa katika jamii husika, tokana na kwamba wazee au wazazi na vijana wanao oana huongezewa heshima katika jamii zao kwa namna mbalimbali. Ingawa jamii zetu za Tanzania (Afrika kwa ujumla) hutofaautina ktk mambo ya kuozana, bado kuna mifano mingi ya kufanana; moja wapo kubwa ni hili la kumtoza mahari kijana anayeoa, 'dowry'.
Historia yatufundisha kuwa hapo zama za kale kijana mwenye heshima na adabu ktk jamii; aliweza kujipatia mke bila hata ya kutoa shilingi. Kuku au mbuzi alitolewa kwa wazazi wa binti kama shukrani kwa kupewa mke. Hii haikuwa na maana kuwa thamani ya binti/mke ni sawa na kuku au mbuzi aliyetolewa kwa wazazi wake, bali SHUKRANI. Hivi leo wazee wanawatoza vijana mang'ombe, na hata mamillion ya fedha, ili kujitajjirisha na kusahau sehemu muhimu ya kiapo cha mapenzi, 'Love'. Je huu ni utajiri wa halali?
Kitendo hiki cha kutoza mahali ni sawa na umilikishwaji wa binti kwa kijana aliyemuoa. Tafsiri nyingi mbaya na mateso makubwa kwa mabinti vinasababisha kurudisha nyuma maendeleo ya wanawake katika jamii zetu. 

Jogoo makunja.

No comments:

Post a Comment